Tuesday, June 18, 2013

Hatimaye Ze Blogger Papaa Kuvinja Ukimya Jumapili hii..

Hello marafiki na wasomaji wote wa Blog hii!!

Leo ninawaletea habari njema  zilizoambatana na mwaliko  maalum kwa watu wote wenye mapenzi mema na Samuel Sasali, The Blogger, MC,Mzee wa Ideas mengi ambaye mara zote husema Mungu alimnyima urefu akamjalia Mdomo (kuongea sana) na kukosa aibu pia!!!

Baada ya sarakasi za kutosha za kutafuta mwenzi wa kumfaa hatimae pacha wangu amegota na kumpata mlimbwende wa pekee aliyewashinda wanawake zaidi ya Bilioni 4 duniani na kuwa wa pekee...Usukani mdogo unaoendesha Merikebu kubwa!!!
 Ndio ni binti huyu Dk Milembe John Madaha ambaye ameteka moyo wa kaka Mkubwa na kwa huyu Papaa amegeuka rapper,mwana mashairi na mtiifu sana!!Kama una kumbukumbu nzuri, blog hii imewahi kum-ZOOM kijana huyu kama mmoja ya vijana wanaopaswa kuigwa na vijana wengine,fuata link umfahamu vema;
.http://chavalamedia.blogspot.com/2012/08/salaam-leo-katika-kipengele-hiki.html
Basi habari njema ndio hii, jumapili hii wewe na wenzako wote ambao ni marafiki wa kweli Samuel Sasali au ni msomaji  wake wa Papaa On Tuesday au ni Mwanachama wa Marafiki Huru au ni mpenzi wa Friends On Friday au umewahi kufundishwa na yeye popote pale,shuleni, chuoni au kanisani au hata kama amewahi kusherehesha shughuli yako yeyote ile..basi sasa ni saa ya kumuunga mkono kwa kumaanisha!!
Ni jumapili hii ya tar 23/06/2013 kuanzia saa nne asubuhi pale Mbezi Beach A katika kanisa la VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE (VCCT),Unaweza ukapanda gari mpaka mwenge na kupanda usafiri wa kanisa unaondoka hapo tatu na nusu ama ukachukua bajaji mpaka huko kanisa la hema,au ukapanda gari mpaka kawe mwisho na kupanda bajaji pia mpaka kanisani au ukashuka Mbezi Tanki bovu na kuchukua bajaji au bodaboda mpaka kanisani...lakini kama unakuja na private car njoo na barabara ya Mwai Kibaki(zamani old bagamoyo road) kisha baada tu ya daraja utaona kibao kushoto kwako kama ukitokea mwenge then fuata njia hiyo kwa hakika huwezi kupotea!!

Ni marufuku kuja mikono mitupu na ni marufuku kuja peke yako,namaanisha jaribu kubeba zawadi ya pongezi na usiache kuwajulisha wengine wanaomfahamu Papaa!!
Haitakuwa siku ya kawaida kwa hakika maana Papaa ni baadhi ya vijana nguli ambae tayari alikuwa kwenye kundi la ma-senior bachelors na sasa rasmi anaanza kuaga aga kundi hilo....na hata harusi yake itakuwa mwishoni wa October, kama hakutakuwa na badiliko lolote basi itakuwa 26TH OCTOBER.. hivyo mwenye macho na asome na kuelewa!!!
Mimi binafsi kwa niaba yangu mwenyewe na kwa niaba ya Blog hii na wafanyakazi wote wa Chavala Ideas Platform ninatamka baraka nyingi kwa rafiki yangu mkubwa na pacha wangu Samuel pamoja na Shemeji yangu,his wife to be ....Mungu awaonekanie katika kila hatua ya michakato hii mpaka hapo watakapooana!!!


Na kwa hakika tuko bega kwa bega,naam tuko tayari kutoa mchango wowote ule wa hali na mali utakaohitajika ili kufanikisha shughuli hii,KWA HAKIKA NINAMKUBALI SANA PAPAA KWA JINSI ALIVYO NA ALIVYO MCHAKARIKAJI,HE IS AMONG MY BEST FRIEND IN TOWN!!!Kwa wale msiomfahamu zaidi basi msiache kutembelea Blog yake kila siku"samsasali.blogspot.com"


NA MWALIKO HUU NIMEUTOA KWA HIARI YANGU KWA NIABA YAKE,HIVYO KAMA UKIKWAMA AU UKIWA NA SWALI LOLOTE NAMNA YA KUFIKA HAPO KANISANI BASI USISITE KUWASILIANA NASI,NASI TUTAKUSAIDIA KUFIKA!!


+255 713 883 797King Chavala-MC


Source:...http://chavalamedia.blogspot.com/2013/06/hatimaye-samuel-sasali-aka-papaa.html

Papaa On Tuesday…..Unao Uwezo Wa Kuchagua Cha Kufanya Lakini Huna Uchaguzi na Matokeo Ya Kile Ulichokichagua Kukifanya.



Tukiwa bado katika Maombolezo ya Kupoteza ndugu zetu katika Mkoa wa Arusha kwa sababu zinazosadikika ni za kisiasa nachukua fursa hii kuwapa pole ndugu zetu wote ambao wamefariki lakini pia na wote waliojeruhiwa hasa hasa Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha rafiki yangu na mtumishi katika Shamba la Bwana Bw. Amani Golugwa pole sana na “majanga” ya Kisiasa. Nimeamini kweli tunao uchaguzi wa nini cha kufanya lakini hatuna uchaguzi wa kuzia matokeo ya kile tulichokichagua kinapotokea. Ukichagua Siasa basi matokeo ya Siasa ujue huna maamuzi nayo.

Wengi tuko leo hivi tulivyo kama matokeo ya kile ambacho tulikichagua katika maisha, na wakati huo tuliona sie ndio wenye mana kuliko wengine wote wakati wa kuchagua lakini hatukujua kuwa kile tulichokichagua hatuna uwezo wa kuhimili matokeo yake ya kwenye maisha. Wengi wetu wakati tunahimizwa kwenda shule tuliendekeza ubishoo na usharubalo, tulikuwa na uwezo wa kuamua either kusoma ama kuendekeza ujinga wa makuzi wakati huo kwa kufuata mkumbo wa mambo yaliyokuwa yakiendelea. Pengine kila ukikaa unajicheka kwa kile ambacho ulikichagua wakati huo na ukasahau methali ya Majuto ni Mjukuu waliponena wahenga, tulijiona sisi ndio tunaojua kuliko wale waliokuwa wakituasa na kutuhusia. Leo tumekuwa na akili tunatamani zile zama tulizokuwa tunakula chips na kuvaa raba za gharama na kuendekeza ubishoo zirudi tena ili tufanye kweli, lakini wapi kila jambo na majira yake. Wengine tunasoma Elimu za Watu wazima sit u tulikuwa na tatizo la ada kipindi hicho la hasha ila tulipokuwa nacho tulitumia na kilipoisha tukajijutia kwenye maisha.

Kuna mdada mmoja rafiki yangu anaishi kwenye mateso makubwa ya ndoa yake na amebaki kujutia maamuzo aliyoyachagua kuyafanya kisa na mkasa anasema hakujua, kama angelijua angechagua kuendelea na maisha yake kwanza ndipo achague kuolewa akiwa na akili timamu. Majanga mengi sana ambayo tunapitia kwenye ndoa na mahusiano ni kutokana na maamuzi yetu ya kukurupuka, maamuzi yetu ya kujiaminisha kuwa tuko sahihi kuliko wengine matokeo yake tunabakia kufa na tai shingoni. Kwani uwongo??ukikaa mwenyewe hujiambia kuwa laiti kama ungelijua usongechagua kuolewa ama kuoa Fulani kisa na mkasa matokeo ya kile ulichokichagua kwenye maisha. Kuna wengine walitaka kuolewa so kilichotokea wakabeba mimba wakidhani maisha yale ya honey baby and sweetheart yataendelea, kongwa walilojitishwa na nira walizojifunga wamebaki kulilia moyoni, mkiwaona barabarani na kwenye facebook utadhani ni ndoa ya mfano kumbe si lolote si chochote kila mtu analala chumba chake nyumbani hakuna furaha ambayo inadhaniwa ipo wakiwa nje ya mlango wa nyumba yao wakikaa wenyewe wanatamani sana kurejesha maisha siku ambazo walikuwa wanacheka na kwenda kula bata na kuitana majina ya mahaba, leo yamebaki kuitana “wewe”, “Nanii”, “Stella”, “Sultani” dry dry dryyyyyyyyyy. Lady Jay d anasema anatamani kuwa kama zamani lakini ndo zama zimeisha tena maisha yamebaki kuishi kwenye matokeo yake.


Kuna Ofisi Fulani nilifanya kazi zamani kuna jamaa alicha kazi baada ya kupata kazi sehemu nyingine kwa ahadi ya project mpya alipohama kwetu akaenda kwingine ambako huko project ikakosa hela akabaki mtaani akajuta sana kwa uamuzi wake wa kuacha kazi alikuwa na muda wa kuchagua kuacha kazi ama kuanza upya sehemu nyingine matokeo ya maamuzi yetu mengi hayamo ndani ya matakwa yetu. Unaweza kuacha kazi sehemu moja ili ufanye kazi kwingine ukashangaa ulikokwenda ndo unapunguzwa wewe ama unahama nyumba moja kwenda nyingine kumbe unakokwenda ndo kuna zoezi la upanuzi wa barabara unabaki kusema ng’ombe wa masikini hazai. Wengine wamepata watoto mapema si kwa sababu walikuwa wanapenda kuzaa bali bali kilichotokea “ajali” ikasababisha waanze kuitwa “mama” ama “baba” wakati wa kudungunyuana walikuwa wanasikia raha ila ilipofika ujauzito wengine wakasema wakatoe ama wakatoa ujue ulikuwa na uchaguzi wakati wa kuamua lakini ukasahau unawajibika na matokeo ya kile ulichokiamua kwenye maisha yako.

Kuwajibika na matokeo ya yale tunayoyaamua ni wachache wetu wako tayari unapotaka kufanya maamuzi kwenye maisha jua kabisa wewe unawajibika na matokeo ya maamuzi unayochukua kwenye maisha. Kila ambacho unakichagua kukifanya jua kina matokeo na uwe tayari kupokea matokeo ya kile ulichokichagua kukifanya kwenye maisha.

0713 494110

Friday, June 14, 2013

Ibada ya siku tatu kuiombea Taifa Stars



Askofu Mkuu wa Kanisa la Good News For All Ministry,  Charles Gadi, kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali wa dini, leo wameandaa ibada maalumu ya maombi ya wazi ya timu ya Taifa, ‘Taifa  Stars’ ili iweze kuibuka na ushindi kwenye mchezo dhidi ya Ivory Coast  kesho kwenye Uwanja wa Taifa.
Gadi aliwataka Watanzania kuungana pamoja kuiombea timu hiyo, kwani  haijawahi kufika mbali katika mchezo ya kimataifa.
“Tuna imani timu yetu ni nzuri, lakini inahitaji maombi zaidi kwa kuwa inacheza na timu ngumu,” alisema askofu Gadi.
Aliitaka jamii iendelee kufanya maombi na kuhamasisha misaada ya hali na mali kwa timu hiyo.
Wakati huohuo, Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen amewapa wachezaji wake mbinu mpya ya kuwakabili nyota wa Ivory Coast katika mchezo wa kuwania  tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.
Poulsen alisema kubwa alilowafundisha wachezaji wake ni kujiamini  watakapokuwa wakicheza na miamba hiyo ya soka Afrika. “Nimewaambia  wachezaji wajiamini, wasicheze na majina ya wapinzani wao,” alisema  Poulsen.
“Ivory Coast ni timu bora, lakini nimewataka wachezaji wangu waione  kama timu ya kawaida kwenye mchezo wa Jumapili. Jambo la msingi wacheze  kwa kujiamini,” alisema Poulsen.
Source: Mwananchi

Tuesday, June 11, 2013

Papaa On Tuesday.......Msiba Wa Kujitakia Hauna Kilio......Hatujifunzi Kutokana na Makosa

Nina Kila sababu ya Kumshukuru Mungu kwa ajili ya Siku hii ya leo kwa kuweza kunipa Pumzi kuongea na wewe tena, huwa ninahesabu ni neema ya pekee sana kwa mimi kupata fursa ya kuongea na wewe kila iitwapo Jumanne, kuna uwezekano wa mkubwa wa wewe kuamua kusoma vitu vingine lakini kwa ile commitment yako kwenye POT a.k.a Papaa On Tuesday nina kila sababu ya Kukushukuru ni Mungu kupitia mimi huzungumza na maisha maisha yako, yamkini si kwa ajili yako moja kwa moja ila wewe uwe msaada kwa kwengine kupitia POT.

Baada ya kumaliza Safari yangu ya Dodoma weekend hii na kupita Morogoro kwa Masaa machache nilikumbana na kisa cha Kujitakia. Siku ya Kurudi nilidhamiria kurudi na Shabiby siku ya Jumapili, nikiwa na mmoja wa wadau Wakubwa wa Papaa On Tuesday na Blog na Chomoza kwa Ujumla mkoani Dodoma walinishauri ni vema nikakata tiketi Jumamosi sababu Jumapili watu wengi wanakuwa wanarudi dara baada ya Purukushani za Weekend na Waheshimiwa na Biashara mbalimbali kwa ujumla, niliwaambia ninaamini nitawahi na nitakata tiketi. Ilipofika Jumapili mapema nilijongea kwenye kwenye kituo nilipokwenda kituoni kuuliza Tiketi nikakosa, nikaenda basi lenye afadhari nikakosa nikaenda lingine nikakosa Mwisho nikaamua kupanda lililopo, nikakaa siti iliyopo na nikakubaliana na hali iliyopo abiria wengine walikuwa wamesimama na mizigo mpaka hakuna pa kusogea nilijilaumu sana kwa kutosikiliza mawazo ya wale walioniambia nikakate tiketi mapema. Wakati aendelea kuwaza mambo mawili matatu nikajilaumu kwa kuto kujifunza kutokana na makosa hiyo ikiwa ni mara ya pili kama sio ya tatu kutokea makosa yale yale kwa namna ile ile nikakumbuka ni mambo mangapi ambayo either kwa kuto sikiliza sauti ya ndani ama watu wengine nimejikuta katika tatizo na kuahidi kubadilika lakini kwa namna nyingine nikajikuta nimerudia kosa lile lile na kwa namna ile ile niliyoahidi kubadilika na kwa kuwa ni msiba wa kujitakia nimejikuta sina wa kumlilia.


Serikali yetu imejikuta ikisaini mikataba isiyo na manufaa kwa wananchi kwa kudhani tu ina manufaa, tangu enzi za Chief Mangungo na Abushiri tumejikuta tumewakabidhi akina Karl Peters nchini yetu pasipo kutambua makusudi hasa ya Treats ambazo tumekuwa tuki-sign leo hii ardhi inauzwa kwa wageni, gas wageni Tanesco na dowans na Richmond ni yale yale, kwa namna ile ile tuliyokosea hapo awali ndipo tumejikuta nchi ime sign mikataba ambayo haina maslahi kwa wananchi..experience hajawahi kuwa a good teacher kwetu. Kuanzia ngazi ya Serikali Kuu mpaka Halmashauri Ugonjwa ni ule ule na kwa kuwa tunakuwa tumejitakia tumejikuta hatuna wa kumlalia.

Sisi wengi wetu ni wepesi kushawishika na tunashawishika na mazingira na manufaa binafsi tuko tayari sisi tufaidike wengine wateseke lakini matokeo yake yamekuwa sio ambavyo tumedhani. Kila mwaka wa uchaguzi tumekuwatukirudia makosa yale yale kwa namna ile ile unadhani tunajifunza??


Nikiwa Mkoani Dodoma niliwasiliana na mtu ambaye anahisi ameteseka sana na anahitaji kujiondoa uhai wake kwa sababu tu ya mapenzi, kila mara mdada huyu amejikuta akidondokea katika mikono wa "wadungunyuaji" amejiampiza mara kadhaa kuwa hata fall In Love na Wanaume ajabu amejikuta katika makosa aliyoyafanya wakati uliyopita yamekuwa yakijirudia na matokeo ya kudungunyuliwa mara zote limekuwa likijirudia nilishangaa sana kusema amekata tamaa ya kuishi kisa na mkasa ni makosa yake mwenyewe na hana wa kumlilia, nilimwonesha tatizo lilipo na tuliomba pamoja. Wakati wmingine kujifanya wajuaji wa mambo yamepelekea kurudia makosa ambayo tungeuliza na kukubali ushauri tusingedondokea katika makosa yale yale kwa namna ile ile.

Yakini katika Masomo yako kila Semester umekuwa na wakati mgumu kwenye shule si kwa sababu shule ni ngumu la hasha makosa uliyoyafanya mpaka ukapata Supplementary yamekupelekea kudondokea katika matatizo yale yale kimasomo, unakumbuka siku ambayo ulijisikia vibaya mpaka ukasema umejifunza na ukaapa kabisa kuwa sasa umeamua lakini umejikuta unakwama katika tatizo lile lile. Kuna nyakati umejilaumu sana kwa kuwa ni msiba wa kujitakia na shule imekuwa ngumu kwa sababu kichwa kimelemewa na mambo mengiiii.


Maisha ni Kujifunza na Maisha ni Kubadilika. Kurudia kosa lile lile ambalo uliwahi kulifanya na kutubu, na kutoa machozi na kujiapiza kutokulirudia tena na umejikuta umerudia kosa lile lile ila kwa kadri ambavyo umekuwa ukirudia kosa lile lile volume ya maumivu inatofautiana kila iitwapo leo, yamkini kosa lilipotokea ulijisikia vibaya ila lilipojiurudia tena maumivu yalipungua hayakufanana na yale ya awali. Kufanya kosa sio Kosa ila kurudia kosa lile lile kwa namna ile ile tena kwa kujitakia inabidi ujihoji kwanini limetokea na wapi umekosea ili kuweza kubadilika. Msiba wa Kujitakia hauna majonzi. Ni mara ngapi umesema utaanza mazoezi ya kupunguza unene ambayo ulipofanya ukapungua lakini ukarudia kula vyakula vile vile, na mwili ukarudi vile vile. Ni mara ngapi ulimejikuta umetumia fedha zako vibaya na kujiapiza kuwa hauta rudia tena kurudia kosa ulilolifanya kutmia fedha vibaya, ni mara ngapi umejikuta LUKU imeisha na umelala giza na kuapa haitatokea tena kwenye maisha, ni mara ngapi umejikuta umerudia kosa lile lile kwa namna ile ile?Wengine wetu kwa makosa yale yale na namna ile ile wamejikuta wakipoteza maisha, kupitia maisha ya wengine nasisi tumejikuta tumedondokea katika makosa ambayo hatuna wa kumlaumu kwenye maisha.

Think Differently and Make a Difference 

0713 494110

Thursday, June 6, 2013

Jitambue Ya Chris Mauki....MAMBO 7 AMBAYO MARA CHACHE SANA UTAAMBIWA AU KUYASIKIA KUHUSU MAHUSIANO/NDOA

1. Yamkini ipo siku utaamka katikati ya usiku wa manane na kumtazama aliyelala pembeni yako (ambaye labda unamuita au anajiita mpenzi wako) na kujiuliza “hivi maisha haya na huyu mtu ndo hadi kifo kweli?” (ukitamani walau kuwepo na kaupenyo kakutokea)

Swali hili linasababishwa na aina ya maisha mnayoishi, yamkini penzi mlilokuwa nalo awali haulioni au wote hamlioni tena, imebaki kuonekana tu na watu wa nje kama mnaopendana kumbe ukweli ni kwamba mnaishi tu pamoja “not as lovers but as in mates”. Zile zama za kuitwa jina lako la kwanza, na yale majina mengine kama darling, honey, sweet heart zimefia mbali na nafasi yake imechukuliwa na majina kama ‘mama nanihii’ baba naniii’ we nanihii’ eti nanihii’ eti wewe’!!! Ile ‘chemist’ au ule mvuto wa ndani ambao ulikuwa unausikia kutokea moyoni hadi katika mifupa yako mtu huyo akiwa karibu na wewe hauioni tena badala yake, akiwepo karibu ndio unaona bora awe mbali. Kipindi hiki mtu huyu akisafiri hutamani arudi, kila siku unamuuliza “unarudi lini eti?” sio kwa kusukumwa na hamu ya kutaka arudi mapema bali kwa kusukumwa na hamu ya kutaka kusikia yamkini kaongeza siku au amepata safari nyingine ya gafla ili uendelee kufurahia kutokuwepo kwake.


2. Maranyingine utajikuta inakulazimu kufanya kazi ya ziada kuliko uliyowahi kudhania katika kuhakikisha penzi lenu linasonga
Yamkini ulifikiri kuwa itakuwa rahisi mara ukikubali kuingia kwenye mahusiano na huyo mpenzi wako. Umetamani kuwa nae kwa muda, umemtafuta kwa muda na sasa ukafikiri mkiamua kuanza mapenzi pamoja ‘things will go smooth’. Mnakuja kugundua kuwa ninyi ni watu wawili tofauti, kila unachokipenda na kukitamani mwenzako hakithamini. Yale uliyokuwa ukiyaamini kama misingi ya mahusiano bora huyaoni kwenye mahusiano yako. Kila ulichowahi kukisoma, kujifunza au kuambiwa kuhusu kuyafanya mahusiano yawe paradiso unaona hakifanyi kazi kwenu. Matarajio yako makubwa kwenye mahusiano yenu na mustakabali wenu yanaingia ukungu na mbele yako huoni hata chembe ya mwanga. Sasa unajikuta ulichodhania ni rahisi kumbe sio, na unalazimika kujituma zaidi, kufanya kazi zaidi na kutumia muda yamkini kuliko mwenzako kuhakikisha mnaweka sawa mambo yenu ili angalau maisha yaendelee. Kuepuka hili nivema tunapoingia katika mahusiano tusiwe na matarajio makubwa kupitiliza na yasiyo tekelezeka ‘overambitious and unrealistic expectation’ Penzi peke yake ndilo litupeleke katika mahusiano kwa kiu ya kusaidiana kuhakikisha raha ya kilammoja inawezeshwa, sio kwa kiu ya kutimiziwa kiu zako tu ‘this is ultimate selfishness’


3. Zipo nyakati unaweza kujikuta unaenda kitandani ukiwa na hasira, na yamkini ukaamka asubuhi ukiwa na hasira zaidi ya ulizo lala nazo.
Tofauti baina ya jinsia hizi mbili kama nilivyogusia kwenye jambo la pili ziko katika maeneo mbali mbali ya mahusiano yetu na mojawapo ni tofauti tulizonazo baina ya wanawake na wanaumehususani katika kuishuhulikia migogoro inayoibuka ndani ya mahusiano yetu. Yawezekana wewe ni mmoja wa wale wasio na hasira sana, muelewa, mwepesi wa kusamehe na kuchukuliana na hali, mara kwa mara unatamani mliongee jambo lililoleta utata baina yenu kabla halijakuwa kubwa na kuleta madhara. Tabia hii ni nzuri sana, lakini kwa bahati mbaya unakutana na mwenzako ambaye hakufunzwa vyema namna na jinsi ya kuishuhulikia migogoro. Unajua katika makuzi yetu wako ambao wamekuwa katika mazingira ambayo hayakuwaandaa kabisa kuja kuhusiana na bina damu mwingine yeyote, tabia zao wanazijua na kuziweza wao peke yao, ni ngumu hata kukaa na mtu huyu kwa lisaa limoja chini ya dari moja, katika saikolojia tunawaita “difficult personalities”. Unakuwa na mtu kama huyu kazini, kwa jinsi unavyoona tabia zake katika kuhusiana na wengine unajiuliza hivi mpenzi wake anaziweza vipi tabia zake? Sasa aina hii ya mtu unajikuta kwa bahati mbaya au nzuri labda ndio umehusiana naye katika mapenzi, kilasiku unategemea kuona mabadiliko lakini ndo maudhi yanazidi. Hata pale anapokuahidi kujitahidi kubadilika ili kukuridhisha bado unaona kama anaongeza machungu moyoni mwako. Kila siku unaona ‘bora hasira ulizokuwa nazo jana’. Ili kuepuka hali hii, kuwa macho sana wakati wa mahusiano, viko vitu vingi sana vya kuangalia katika tabia za mtu kabla hujaamua kuanza naye mahusiano ya kimapenzi. Hii habari yakujipa moyo na matumaini yasiyo rasmi eti ‘atabadilika tu!!’ ‘nitajitahidi kumrekebisha’…. ‘Mungu atambadilisha’ . Wengine wameshindikana tangia kwao tokea utoto we umekutana naye juzi tu utamuwezea wapi kama sio kujinunulia kitanzi kwa hela yako mwenyewe? Wako wengi waliotarajia hivyo hivyo kuwa wapenzi wao watabadilika sikumoja, bahati mbaya walipoamua kurasimisha mahusiano yao na wengine kuingia kwenye ndoa tabia ndo zikazidi kuwa mbovu na za kukatisha tamaa. “usijaribu kina cha maji kwa kuingiza mguu” Watch out


4. Utakuja kugundua kuwa jitihada za kufanya mambo kivyako hazifanikiwi na sio muhimu kama pale ambapo mnaweka nia zenu pamoja.
Katika mikiki mikiki ya kushindana katika namna mnavyoishuhulikia migogoro yenu, yamkini baada ya kuona mambo hayaendi unaamua kujichukulia njia zako mwenyewe, humshirikishi mwenzako chochote, maamuzi yako ni yako binafsi na wala hutaki kusikia chochote kuhusu yeye. Yamkini ameamua kukuacha uendelee vile ulivyoona inafaa au labda bado hajakubaliana na uamuzi wako wa kujitenga na kuanzisha maisha binafsi ingawa bado mko chini ya dari moja. Katika yote haya utakuja kugundua mambo mengi hayaendi kiufanisi sana au labda yanatumia jitihada na nishati kubwa zaidi tofauti na pale ambapo yangehusisha nia zenu pamoja. Najua unaweza kusema ‘je kama hataki nimbembeleze hadi lini?’ lakini ukweli nikwamba usiwe na haraka ya kukimbilia kutapanya bali uwe zaidi na hamu ya kukusanya. Sio mambo yote yanarekebishika kwa usiku mmoja. Inabidi uifanyishe mazoezi misuli yako ya uvumilivu ili ikuwezeshe kustahilimi, ndani yako ukiwa na tumaini la kuuona mwanga na sio kiza. Kama wako waliowahi kuitafuta furaha iliyopotea na wakaiona, kwako pia inawezekana.


5. Mahusiano bora haimaanishi ni mahusiano yasiyo na migogoro wala mikwaruzano bali ni mahusiano ambayo wanaohusiana wameamua kuwatayari katika jitihada endelevu kuhakikisha kilakitu ndani ya mahusiano yao kinakwenda sawa.

Yamkini umewahi kudhani kwamba mahusiano bora ni yale ambayo mtajiepusha wakati wote na katika yote kuingia kwenye migogoro na mikwaruzano. Labda umewahi kujipanga kufanya hili mara uingiapo kwenye mahusiano au kutarajia hili toka kwa mpenzi wako na mara unapoona alama au dalili za migogoro basi unahisi kuwa uko katika mahusiano potofu nakutafuta njia za kujihadhari nayo. Napenda kukupa taarifa tu kwamba matarajio hayo ni matarajio hasi. Unahitaji kuya badilisha na kuwa na matarajio chanya yatakayo kuwezesha sio kukwepa na kuikimbia migogoro bali nyie wawili kwa pamoja kujua vyanzo vya migogoro yenu na namna bora itakayowawezesha kukabiliana nayo, kila mmoja akiwa na nia ya dhati na jitihada endelevu kuhakikisha mnalilinda penzi lenu dhidi ya kila pepo zitokazo ndani ya mahusiano yenu au nnje yake. Jitahidini wote kuwa na mtazamo huu kwasababu mara anapokuwa nao mmoja baina yenu inakuwa kazi sana pale ambapo mwenzako anaangalia suala la kutofautiana kwenu tofauti kabisa na wewe unavyoliangalia, na utaona matokeo yake pale mnapo tofautiana kwenye wazo au jambo fulani. Wakati wewe ukijitahidi kutafuta namna ya wote kusuluhisha na kuendelea mbele, yeye anakuhimiza kuwa mahusiano yenu hayakuwa mpango wa Mungu na kwahiyo kila mmoja atafute hamsini zake. Kwa tabia hii mtu kama huyu hawezi kamwe kutulia kwenye mahusiano bali anakuwa mtalii kutoka mbuga moja ya mahusiano kwenda mbuga nyingine, na wakati huo moyoni mwake kila mara akidhania labda mbuga inayofuata ni nzuri kuliko aliyopo.


6. Utakuja kugundua kuwa jitihada za kumbadilisha mpenzi wako kitabia zinakwama na kukuwia ngumu kuliko jitihada za wewe mwenyewe kubadilika.

Yamkini mlipokuwa mnaanza mahusiano au hata kabla hamjaamua kuanza mahusiano ulikuwa unaona baadhi ya tabia zake, nyingine hukuzipenda lakini kwasababu ya penzi ukazifumbia macho ukijipa matumaini zitabadilika mbele ya safari, au penzi litazifunika au labda utajitahidi kumbadilisha na kwasababu anakupenda atakubali kubadilika. Kwa bahati mbaya baada ya kupiga hatua za mapenzi mbele, kila unapoangalia mabadiliko ya zile tabia unaona hakuna kinachobadilika, na sasa hivi unashindwa kuzifumbia macho tena kama zamani, kila unapoziona unalazimika kuongea na kujibizana na kutaka akuhakikishie kuwa atabadilika. Yawezekana umeshaahidiwa mara nyingi tu “nakuahidi nitabadilika mpenzi” lakini wapi!!!! Ukijiangalia wewe ndio umekuwa kiongozi wakumbadilisha mwenzako kitabia, hadi akikuona anakuogopa kama mwanafunzi na mwalimu wake, tena mbaya zaidi ukute wewe ni aina ya wale ambao wakiona kosa hawalinyamazii hata dakika mbili hata kukiwa na wageni au marafiki, mtu anapewa vipande vyake ‘on the spot’. Bahati mbaya ni kwamba utajaribu sana kushindana na tabia zake hadi utakapo fikia uamuzi wa wewe kuangalia ni maeneo gani kwenye maisha yako ambayo ukijaribu kubadilika yanaweza kupelekea pia mabadiliko upande wa mwenzako katika hali chanya.

7. Kwa jinsi utakavyokuwa ukijitahidi kuzikabili hofu zako na changamoto nyingine katika kuyafanikisha mahusiano yenu ndipo utakapogundua uhalisi wa jinsi wewe ulivyo.

Maranyingine ni ngumu kujifahamu uhalisi wa vile ulivyoumbwa na jinsi tabia zako za asili zinavyojidhihirisha. Yamkini unadhani kuwa wewe ni mwema sana kumbe sivyo watu wakuonavyo nje. Tunaambiwa kwamba maranyingi mtu anapokamuliwa hadi tone la mwisho ndipo tabia yake halisi huonekana. Hali kadhalika katika mahusiano yetu ya kilasiku baina yetu na wale tunaowapenda. Labda unapicha fulani akilini mwako na unadhani wote wanakutazama hivyo, yawezekana ni picha nzuri au mbaya, wewe wajua. Ukweli ni kwamba kwa kadiri tunavyozikabili hofu zetu za kila siku katika mahusiano yetu na kwa jinsi tunavyokumbana na changamoto na kuzishuhulikia ndipo tunaujua uhalisi wa jinsi tulivyo, na pia ndivyo mwenzako anaweza kukusoma kinagaubaga namna na aina ya mtu anayehusiana naye. Kumbuka yamkini haya yasiwe matatizo bali changamoto tu.

MWISHO:


Wednesday, June 5, 2013

CHRISTINA SHUSHO DISSES TOP KENYAN GOSPEL ARTISTS :What’s cooking?


Gospel music is currently the biggest industry in Kenya with the likes of booty shaking size 8 and Lady B who was Nonini’s former girlfriend crossing over. But is it because of the money in the JESUS INDUSTRY because some Gospel artists are getting huge sums of money and endorsement in big companies like Malta Guiness which endorsed the famous Kuna Dawa hit maker Esther Wahome? which leaves one wondering is there healing in the malta beer. Not forgetting the Gospel jam sessions held in clubs where secular dance moves rule and if u have ministering song you won’t be invited for example the likes of Mr Googz who is a strong critique of secularism in gospel with his GOSPEL CELEBRITY song being denied airplay by many Gospel djs.
Of late another top Gospel Artist from Tanzania Christina Shusho of NIPE MACHO hit has come out to criticize Kenyan gospel artists.   She says that the Kenyan gospel industry is more of a business than a Ministry. The well known Shusho who is strict on faith says that most artists are preaching water and drinking wine. Not forgettting Ringtone, Astar, Holy Dave and the list is endless who have been caught in clubs regularly.  Shusho tells the Kenyan Gospel Artists to repent and come back to God instead of concentrating on the money and fame which are all vanities. She also talks of the dance moves in churches which are club related and contains alot of satanism. The ever smiling Christina Shusho says that  most of the Kenyan Gospel Artists lack mentors and they are church hoppers.
Christina  Shusho further  advises recognizes some of the Gospel artists  like Mary Atieno Geraldine Odour and Daddy Owen who are clean in the public eye and out to win souls. Will Kenyan Gospel Artistes wake up to reality and transform or will they claim that you shouldn’t judge a book by its cover as they always say. Keep it Uhondo254 for more.

Source: Uhondo254 blog

Tuesday, June 4, 2013

Solomon Mukubwa Kuachilia Albam Ya Sifa Za Mungu Mwezi June, 2013



Mwanamuziki Wa Injili Mwenye Asili ya Kongo na Mwenye Maskani nchini Kenya Solomon Mukubwa ameieleza blog kuwa anatazamia kuachilia Albam yake yenye Jina la Sifa Za Mungu ndani ya Mwezi huu June, 2013.

Solomon Mukubwa aliongea na Blog hii wakati huo akiongea na Kipindi Chako mahiri Cha Gospel "Chomoza" mwishoni Mwa wiki alipokuwa akifanya mahojiano.

Hii inakuwa ni Albam ya Tatu Kutolewa na Solomon Mukubwa.

Papaa On Tuesday...Hata Kama Tutabanana Hapa Hapa Atapata Aliyejaaliwa...2

Ikiwa Mwezi wa 5 umekwisha malizika sasa tunaingia mwezi wa 6 ambapo itakapokuwa imefika mwishoni basi mwaka utakuwa umeshafika nusu na Serikali itakuwa inaingia katika Mwaka mwingine wa fedha ni heri ukaendelea kujipanga. Kwa wale wanaofatilia issue ya mabadiliko ya rasimu ya Ujio wa katiba mpya wanaweza kutoa maoni yao kipindi hiki kwa utaratibu wa Tume kabla Rasimu haijaingia katika Mchakato wa Bunge la katiba. Leo ninaandika mwendelezo wa Papaa On Tuesday niliyoiandika mwezi August Mwaka 2012 hasa baada ya wiki hii kuwa busy na Finalists wa vyuo vikuu na kuongea nao ndani ya wiki hii nimeongea na wanafunzi wa DIT, NIT, UDSM Mabibo fellowship na kuanzia jana Jumatatu nitakuwa CBE.

Mtaani kumekuwa na misemo mingi inayoonesha namna ya kung`ang`ania kile unachokiamini,mojawapo ya misemo hiyo ni kama ipo ipo tu, msemo mwingine ni Tutabanana Hapa Hapa. Wiki chache nikiwa katika matembezi yangu ya jioni nikiwa nimekaa na jamaa wa kijiweni pamoja na madereva wa taxi kikatokea kichekesho ambako kalipelekea huu msemo kuusikia. Tukiwa tumekaa akatokea mteja kwa ajili ya taxi karibu madereva 6 walimkimbilia mteja yule, dereva mmoja nilibaki nae pale maskani,yule mteja akawaacha wale wote waliokuwa wakimzonga akamfata yule dereva niliyebaki nae pale chini akamwambia nipeleke. Wakati yule dereva wa taxi akisimama akasema "Hata Wote Tukibanana Hapa Hapa, Atapata Aliyejaaliwa"neno hili likanipa tafakari ya siku baada ya kulisikia.
                                            
Katika Maisha kumekuwa na ushindani wa kila siku, Katika masomo kuna watu wanasoma weeeeeee lakini mwisho wa siku anayejitwalia namba moja ni yule ambaye pengine wala haonekani kuwa na bidii. Katika Kizazi chetu kupata ajira imekuwa ni changamoto unakwenda kwenye Interview una sifa zote na umefanya interview vizuri lakini mwisho wa siku anapata mwingine kabisa. Suala la Biashara nalo ni changamoto kuna watu tunadhani wangefanya vizuri lakini wanafanya vema ni wengine kabisa mpaka wengine wameitwa wana mkono wa biashara.Kuna Wadada kwa jinsi walivyo tulitegemea wao waolewe mapema lakini mambo yako tofauti na vile wale wanaonekana wangechelewa ndio wanao tangulia, itasikia watu wanasema kuna watu wamezaliwa na bahati kwenye maisha wana kismat.

Wenzetu Waislam wamekuwa wakiamini kila mtoto duniani ana riziki yake, kila anayekuja duniani ana share ama ana sehemu katika mgawanyo wa riziki za Mwenyezi Mungu hapa duniani, hata tukibanana namna gani basi kila mtu ana sehemu yake ya kumfanya aweze kuishi hapa duniani. Mtaani kuna maneno kama Ngekewa, Ngekewa maana yake ni kama Nyota kumaanisha kuna watu nyota zao ziko na mwanga sana kuliko wengine. Kwenye Biblia kuna kitu kinaitwa "Kukubalika" ama "Kupata Kibali" kwa lugha ya kimakonde wanaita "Favor". Kibali kinakutofautisha na watu wengi sana kwenye maisha. Na hauhitaji jitihada kukubalika as long as ile neema iko juu yako, ni kama vile samaki asivyopata shida kuogelea ama ndege kuruka hewani ndivyo ambavyo ukiwa na kibali huitaji kuwalazimisha watu wa kukubali. Kuna watu ninawajua kwenye maisha yangu wanafanya kazi kwenye maofisi wao wanapendwa sana na wafanyakazi wenzao, na hii ni automatic hakuwahi kuwalazimisha watu wawapende basi tu inatokea kukubalika, mbaya zaidi kuna watu wanajisikia vibaya eti wewe unavyokubalika utadhani ulifanya application letter ya kukubalika ya kwake ikashindwa. Kuna Ma Mc wengi sana duniani, na kuna wengine Wanavaa sana, kwa kadri wanavyovaa ndivyo wanavyozidi kuwa kero ila kuna watu ambao wanakubalika Wakishika Microphone tu Watu wote Mioyo yao iko tayari kumpokea, huyu mtu amepata Kibali ndani ya mioyo ya watu. Rafiki yangu John Lisu Muimbaji wa Nyimbo za Injili, Sio Kwamba anaiomba Saaaaaaana, au anapiga Ma-cord ya Muziki sanaaaa, John Lisu akishika Gitaa lake akasimama mbele za Watu akianza tu kuimba watu wote wanapokea, Kwanini??huyu Mtu anakibali ndani ya mioyo ya watu. Mwaka huu nikiwa Uwanja wa Taifa katika Tamasha la Pasaka nilishangaa sana aliposhika Microphone Rose Muhando, yaani huyu Mama anaimba nyimbo zile zile ambazo tunazisikia kila send off na harusi tukienda lakini akianza tu kuimba kuna hali ya tofauti hutokea huyu mtu ana Kibali kwenye mioyo ya watu. Haya mambo sio kuimba tu na kwenye maofisi hata kwenye kuoa na kuolewa. Hujawahi sikia watu wanasema "Maharusi Hawaendani" unakuta Mkaka Bongeee la handsome halafu mdada mtu wa kawaida sanaaaaaaa, au unakuta familia moja masikini nyingine ni tajiri kwanini haya huwa yanatokea kwenye maisha??haijalishi watu wako wangapi duniani wanafanya kile kile unachofanya ama wanashinania kile unachoshindania, kama ipo ipo tu.Nimejifunza kuto kukata tamaa katika kile ninachokifanya zaidi ya kukiboresha, huwa siogopi wala sijisikii wivu mbaya kuona kuna mwenzangu anakubalika zaidi yangu, ukiangalia mawimbi yanayokuzunguka utazama kama Petro kwenye bahari. Sitaacha kuwa Mc sababu kuna ma Mc wengi sasa hivi Dar ama Tanzania, Kila Mtu ana Upako wake kuna event ambazo watu wakikaa kwenye vikao watasema tu, atafutwe Papaa, Sitaacha kuwa na Blog eti sababu kuna watu wengi wanafanya Blog, Kila Blog ina upako wake na Kila Mwandishi ana kibali chake, Siwezi jenga fitna kwa mtu ama kuwa na wivu kwa mtu sababu eti yeye anakubalika zaidi kuliko mimi, ninajua hakuwahi fanya application ili akubalike ila Kibali kimemfanya akubalike katika maisha yake. Nimewahi ona Wadada wazuri na warembo wakiwa na shauku ya kuolewa wanabaki king'aa macho wakati wale unaoona ni kituko ndo wanavaa mashela. Hujawahi ona Mtoto wa Masikini anapona Hospital na Mtoto wa Tajiri anakufa hospitali hiyo hiyo??Kizazi chetu kila mtu anatafuta "Kutoka" hata watumishi wa Mungu pia Wanatafuta Kutoka, ukweli ni kwamba ukitaka Kutoka bila kibali inakula kwako, kila unachofanya kitageuka kuwa kero na kila mtu atakuwa anakaa mbali na wewe. Kibali kinawavuta watu kukusaidia na kuwa na wewe. Nimeshuhudia nimekuwa na marafiki wengi wenye kunisaidia katika mambo mengi si kwa sababu ninajua sana ila Mungu amenipa Kibali mimi na Blog yangu. Kupitia Blog hii nimekuwa na Marafiki Ulimwengu Mzima, sio Sumbawanga,, Sio Ukerewe, Sio Namtumbo, Sio Ulaya, America na hata Asia, Watu wamekuwa wakipokea katika Madhabahu hii, sasa kwanini tugombanie fito wakati wote tunajenga nyumba moja??Hata kama tutabanana hapa hapa wote atapata aliyejaaliwa.Mwalimu Wangu Pastor Carlos pamoja na Mwalimu Wangu Mgisa Mtebe Waliwahi nifundisha wakaniambia Kile ambacho unafanya Vizuri na hautumiii Msuli Mkubwa Kukifanya hautumii muda mrefu kukifanya na Unafanya Kwa Ustadi Mkubwa ukiambiwa kukifanya basi Kitazame hicho kwa Umakini. Mwalimu Wangu Mgisa Mtebe aliniambia "Maji hayajitahidi Kulowesha" Mwl. Wangu Carlos aliniambia "Samaki hafundishwi Kuogelea". Mwl. Mgisa aliniambia Yeye akipewa Kuwa Mc Jasho litamtoka Kutafuta Maneno, Ila Kuna watu wakipewa kuwa Ma Mc utashangaa amepata wapi hayo maneno ya kuongea. Kuna watu wako talented hata kuwaza, wakati wewe haujawaza hicho kitu yeye alishawaza kitofauti zamaniiiii. Kila mtu Mungu amempa fungu lake. Ukiona Kuna Kitu unatamani Kukifanya halafu unapata nacho sana tabu kujiandaa ili ukifanye basi jiulize mara mbili mbili. Kuna watu wanashangaa Papaa Unapata wapi Uwezo  wa Kuandika Papaa On Tuesday Kila Jumanne, Ukweli ni Kwamba Mimi Ninawashangaa wale wanaonishangaa Sababu nina Papaa On Tuesday nyingi mpaka nashindwa ipi niandike, Kwa Mwaka kuna majuma 52 ina maana Kwa Mwaka Ninaandika Papaa On Tuesday 52 na tangu nianze kuandika huu ni mwaka wa 3, Mimi nashangaa Wale wanaoshangaa. Mungu amenipa hiyo nafasi ni kazi yake kunipa cha Kuandika na sio mimi kutoka na Jasho. Nisipo kuwa na cha kuandika jumanne naumwa nakosa raha kabisa.
Hata kama tutabanana hapa hapa atapata aliyejaaliwa. Mungu yuko tayari kukupa Kibali katika eneo ambalo amekusudia kukutumia,utalazimishia mambo sana kwenye maisha "Neema" ni mafuta ya griss katika Vyuma. Mungu atusaidie. Usijisikie vibaya unapoona mwenzako anapata wewe unakosa na wakati mwingine unaona wale unaowawazia mabaya ndio wanapokea wewe hata chembe haupokea "God's time is the best time". Wakati wa Mungu Ukifika kwenye maisha yako milango itakufungukia mpaka utashangaa, hakuna umri kupita kama kusudi bado lipo kwenye maisha. Kuna wanawake wengi sana nimefahamiana nao duniani lakini nimemchagua Milembe John Madaha hata ukiuliza ilikuaje kuaje siwezi kupa jibu la kuridhisha ila ukweli ni kwamba hata kama watu watabanana hapa mjini lakini atakayepata ni yule aliyejaaliwa kupata.

Think Differently and Make a difference.
Papaa Ze Blogger.
0713 494110.

Monday, June 3, 2013

Apostle Ndegi Awataka Watumishi Kufanya Mazoezi



Apostle Onesmo Ndegi wa Kanisa la Living Water Worship centre alimaarufu Makuti Kawe amewataka Watumishi wa Mungu Tanzania na Ulimwenguni Kote Kufanya Mazoezi Ya Mwili kwa ajili ya Kulinda afya zao ili Mungu azidi kuwatumia zaidi.

Apostle Ndegi alisema hayo alipokuwa akiongea na Kipindi Nambari One Cha Gospel Tanzania "Chomoza" Jumapili hii wakati alipohojiwa wakati alipokuwa akifanya mazoezi katika gym.

Alisema Roho Mtakatifu anatuelekeza tutumie vizuri hekalu lake zaidi ya utakatifu lakini pia kuutunza mwili kwa kuuweka ukae fit na kuepuka kula hovyo wakidhani ndio baraka.

Martha Mwaipaja na Christina Shusho Waingia Kwenye Kinyang'anyiro Cha Africa Gospel Music Awards


Kwa Mara Ya Kwanza Tanzania imeingiza wanamuziki Wawili katika Kinyanganyiro Cha Africa Gospel Music Awards. Kwa Miaka Miwili Mfululizo Mwanamuziki Christina Shusho pekee ndiye aliyeingia Katika Kinyang'anyiro hicho ambapo mara zote 2 hakuweza kufanya Vizuri Mwaka huu Christina Shusho Pamoja na Martha Mwaipaja Wameingia Katika Kinyang'anyiro hicho.

Mwaka Jana Umoja Wa Bloggers Uliamua kumuombea Kura Christina Shusho kwa ajili ya Tuzo Hizo na Mwaka huu Media Za Kikristo Zitaungana Kwa ajili ya Kuwaombea Kura watanzania.



Namna ya Kupiga Kura
1. Click hapa...http://www.africagospelawards.com/nominations.html

2. Kisha Bonyeza Kitufe Chenye neno "Vote".

3. Utaingiza Email address yako.

4. Kisha utafuata maelekezo.

Mimi Nimesha Vote...Kazi Ni Kwako.


Thank you for voting on BallotBin!
Your vote has been recorded.

Your receipt number is: 430
The secret word for this receipt is: deduce
Please support our free service by visiting our sponsors.

You may not view the results of this bin


Christina Shusho atwaa Tuzo Za Grooves Music Awards Mwaka 2013


Mwanamuziki Wa Injili Christina Shusho kwa Mwaka wa 3 Mfululizo ametwaa Tuzo za Grooves Music Awards zinazoandawali nchini Kenya na Mwaka Huu Mgeni Rasmi akiwa Mhe. Rais Kenyatta.

Hii Ikiwa ni mara ya tatu Mfululizo kwa Christina Shusho kupitia grooves music awards amezidi kuwaacha mbali wanamuziki wa Tanzania walioshindanishwa na yeye. Mwaka Huu katika Kundi la Tanzania Christina Shusho alishindanishwa na Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Martha Mwaipaja, Rose Muhando,Upendo Nkone na Shusho kuibuka Kidedea katika kundi hilo.

Grooves Music Awards ni Tuzo zinazotolewa Kila Mwaka Nchini Kenya ambapo Wanamuziki wa Nchini Kenya na nchi Jirani hushindanishwa.

Tuzo za Tanzania Gospel Music Awards kwa zilifanyika miaka 3 iliyopita..



MALE ARTIST OF THE YEAR
DK Kwenye Beat
Eko Dydda
Jimmy Gait
Kevoyout
Kris Eh Baba
Willy Paul
FEMALE ARTIST OF THE YEAR
Eunice Njeri
Gloria Muliro
Hellena Ken
Jemimmah Thiong'o
Mercy D'Lai
Mercy Wairegi
GROUP OF THE YEAR
BMF
Christ Cycoz
Kelele Takatifu
MOG
SOC (Saints of Christ)
Tetete
NEW ARTIST OF THE YEAR / GROUP OF THE YEAR
Bahati
Chuchu
Denno
HopeKid
Joyce Omondi
Makenna
VIDEO OF THE YEAR
Conquerer - Joyce Omondi
Emmanuel - Mercy Masika
Katikia Yesu - Kris Eh Baba
Mbona - Daddy Owen & Dennoh
Money Money - M.O.G
Sari Sari - DK Kwenye Beat ft. Anto Neo Soul
SONG OF THE YEAR
Appointment- Jimmy Gait
Mbona- Daddy Owen ft. Dennoh
Mpango wa Kando- Gloria & Evelyne
Sari Sari - DK Kwenye Beat ft. Anto Neo Soul
Sitolia - Willy Paul & Gloria Muliro
Wanajua - Pitson & Mwenye Haki
WORSHIP SONG OF THE YEAR
Asante - Chomba
Ayala - Mercy Wairegi
Hutaniacha - Makenna
Nibariki - Rozy Ohon
Nimekubali - Eunice Njeri
Usinipite - Ali Mukhwana
ALBUM OF THE YEAR
BMF - Rise Up
Dennoh - Naona Mbali
Mambo Yanabadilika - Hellena Ken
Nuru - Mercy Wairegi
Penya - Jemmimah Thiongo
Urban Prayers - Rigga
HIP HOP SONG OF THE YEAR
Beautiful People - Eko Dydda
Bila Yesu - SOC
Bonga Bonga - Kelele Takatifu
Champion - Christ Cycoz
Katikia Yesu - Kris Eh Baba
Sina Chorus - Rigga
AUDIO PRODUCER OF THE YEAR
Bizzy B
Dr. Eddie
Gitonga
Jackie B
Saint P
Teddy B
VIDEO PRODUCER OF THE YEAR
Dr. Eddie
Eagle Films
J Blessing
Princecam
Tiger
Young Wallace
RAGGA / REGGAE SONG OF THE YEAR
Amazing Grace - Guardian Angel
Get Ready - Jfam
Holiday - Hope Kid
Monday till Sunday - Dafari
Pull Up - Kevoyout
This Life - Redemption ft. Simbo & Guardian Angel
COLLABO OF THE YEAR
Holiday - Hope Kid & Altermin Dancers
Kando - Gloria Muliro Ft. Everlyne
Kofi Yoo - Masterpiece ft. D.K Kwenye Beat & Cabassa
Mbona - DaddyOwen Ft. Dennoh
Sitolia - Willy Paul & Gloria Muliro
Wanajua - Pitson & Mwenye Haki
DANCE GROUP OF THE YEAR
Alabaster
Altermin
Flamers
Iced
Jims & Dims
Zionists
GOSPEL RADIO SHOW OF THE YEAR
Gospel Sunday - Milele FM
Inuka - Hot 96
Replay Show - Truth FM
Shangilia - Hope FM
Trinity Connect - HBR
Tukuza - Radio Maisha
RADIO PRESENTER OF THE YEAR
Allan T - Trinity Connect (HBR)
Amani - Shangilia (Hope FM)
Antony Ndiema - Tukuza (Radio Maisha)
Kambua - Inuka (Hot 96)
Esther - FNL (Ghetto Radio)
Jay Njoroge - Mwamba (HBR)
DJ OF THE YEAR
DJ GG
DJ Krowbar
DJ Mo
DJ Sadic
DJ Sanch
DJ Touch
GOSPEL TV SHOW OF THE YEAR
Crossover - NTV
Gospel Garage - K24
Kubamba - Citizen TV
Password - NTV
Rauka - Citizen TV
Tukuza - KTN
PWANI SONG OF THE YEAR
Calender ya Mungu - Anastacia Mukabwa
Chuna Pua - Kimsa
Elshadai - Yvonne Aphia
Maisha Bila - Princess Farida
Nakuabudu - Clemence Tumaini
Nakungoja - Mercy D Lai
RIFT VALLEY SONG OF THE YEAR
Ashe Papalai - Charity Tajeu
Kiboiboi - Faith Kosgei
Maiwek - Joel Kimeto
Osalaba - Sam Manga
Safina - Maryanne Tutuma
Young Man - Mr. Israel
WESTERN SONG OF THE YEAR
Chemishet - Doreen Baruto
Matsai ka Yesu - Gloria Muliro
Nge Ekhisi - Selina Sitati
Olwanda - Sally Siboi
Omusamba Kwa Yesu - Bishop Olumasa
Shibenganyata - Joesph Sishia
EASTERN SONG OF THE YEAR
Kwambata - Dorcas Ndambuki
Ndikasyoka Thinani - Stephen Kasolo
Nibwega - Kendi Meme
Nue Ndete - Mbuvi
Twendaneni - Ameru Crew
Utao - Purity Katieko
NYANZA SONG OF THE YEAR
Amiela Miela - Wamor
Inkanye Nyasae - Caro Nyakwaka
Kwe Kende - Rosemary Ogonya
Many Many - Tetete
Nying Manyien - Geraldine Oduor
Sonko wa Sonko - Christine Atieno
CENTRAL SONG OF THE YEAR
Agocwo - Betty Bayo
Dady Wa Power - C-Bsir
Kindu wa Nii - Dennis Mutara
Kiriro - Simon Njehia
Magegania - Sammy Irungu
Ruciu Rwaku - David Mambo
ARTIST OF THE YEAR (UGANDA)
Coopy Bly
Exodus
Holy Keane Amooti
Jackie Senyonjo
Ruyonga
Wilson Bugembe
ARTIST OF THE YEAR (RWANDA)
Bahati Alphonze
Gaby Irene Kamanzi
Theo Uwiringiye
Tonze
Kabaganza Liliane
Patient Bizimana
ARTIST OF THE YEAR (TANZANIA)
Bahati Bukuku
Bonny Mwaitegi
Christina Shusho
Martha Mwaipaja
Rose Muhando
Upendo Nkone
ARTIST OF THE YEAR (BURUNDI)
David Nkundimana
Dudu Niyukuri
Fabrice Nzeyimana
Fortrand Bigirimana
Redemption Voice
Seraphins Song

SARA K: Uchuuzi Wa Mboga mboga Ulimuingiza Studio




Sarah K akiimba kwa hisia


SARAH K ni muimbaji anayegusa watu wengi hasa kutokana na nyimbo anazoziimba, lakini ni wachache sana wanaofahamu historia ya muimbaji huyo.

Muimbaji huyo aliyezaliwa miaka 42 iliyopita, ameolewa na mchungaji japo kabla ya kuanza huduma ya uimbaji, alishafanya jitihada nyingi maishani ikiwemo kuuza mbogamboga ili mradi maisha yasonge.
Makala haya yanaangazia maisha na mapito magumu aliyoyapitia muimbaji huyo kabla ya kuinuliwa na Mungu.

Kabla ya kuanza huduma ya uimbaji, Sara ambaye jina lake kamili ni Sarah Kiriare alikuwa akikusanya fedha kidogokidogo ili apate kuingia studio, ambapo alikuja kufanikiwa na kutoa albamu kwa lugha yake ya asili.

Mbali ya changamoto mbalimbali alizowahi kupitia ikiwemo kukatishwa tamaa na baadhi ya rafiki zake tena wa karibu, ikiwemo kudai kwamba sauti yake haifanani na uimbaji na kwamba ni kama vile anaongea na si kuimba na pia wengine wakisema sauti yake ni ya kiume, jambo ambalo kwa kweli lilimhuzunisha sana, lakini yote hayo hayakumzuia kusonga mbele.

Pamoja na kudharauliwa na kuonekana hafai kwa baadhi ya waimbaji ambao kwa namna moja au nyingine amewafanya kujulikana mbele ya jamii, pia ni jambo ambalo Sarah anaguswa nalo moja kwa moja.

Sarah anasema kuwa suala la kudharauliwa lilikuwa likimliza na kuamua kumlilia Mungu hadi kufikia hapo alipo; ni matokeo ya kusema jambo linamlomsumbua kwa Mungu wake, mathalan msanii mmoja aliyewezeshwa kupitia Sarah, na kisha baada ya hapo maneno yakaanza, ikiwamo kudai kuwa Sarah si lolote wala si chochote kwa maana hajawika kama ambavyo muimbaji huyo aliyewezeshwa kutoka anavyowika.

Muimbaji huyo ameshawahi kuuza nyanya, magunia, kutembea kwa mguu kwa kukosa nauli, kuimba kwa kukopa pesa ya studio na albamu haitoki kutokana na kuwa na deni kubwa, kutembeza kanda mguu kwa mguu.
“Niseme tu nimeshapitia maisha magumu; nimeshauza nyanya, nimeuza sukuma, nimeuza mangurunya, nimetembea mguu yaani kwa miguu bila ya kupata hela ya kwenda na gari.

“Nimeanza kuimba kwa kukopa pesa; naomba pesa za studio; naenda halafu siuzi kwa hivyo nadaiwa hizo fedha sijui nizitoe wapi.
Nimeshalia, nimeshatembeza kanda zangu zikiwa mfukoni nikipeleka kwa wenye maduka yaani mambo yalikuwa magumu mpaka mahali Mungu akanifikisha nasema asante.”



 Sarah K akiwa katika pozi na mwanae

Sarah K ameolewa na ana watoto watatu na anasema kuwa yeye ni Mkenya; anaeleza sababu za watu wengi kulia akiimba nyimbo zake: “Nimeshaona hivyo tena mara nyingi nikienda kwenye kanisa ambako ninakwenda kuhudumu, ninajikuta hata mimi mwenyewe nalia, kanisa pia hata watu wengi wanalia nadhani kwa sababu wanapata mguso ambao pengine kuna mambo walishapitia, pengine wamekata tamaa yaani ile basi kama vile wanaona Mungu amewasahau lakini niwaambie kuwa Mungu anatuambia tusishughulike sisi wenyewe tusije tukafichaficha au tukajifanya hatutaki kuyataja, tumwambie waziwazi ndivyo ninavyoomba yaani nikulisema linalonitatiza,” anasema.

Sarah K aliyeanza huduma ya uimbaji mwaka 1991 ambapo alitumia lugha yake ya asili na kufanikiwa kutoa albamu tatu kwa lugha yake.

“Nina albamu kama tatu hivi za kilugha halafu mwaka wa 2000 ndio nilitoa albamu ya kwanza iliyokuwa inaitwa Wamtumainio Bwana na Mwimbieni Bwana nyimbo kama hizo. Halafu mwaka 2003 ndio nikatoa albamu ya Milele Daima na ndani yake ndio kuna wimbo ‘Nasema Asante’.

“Hivyo ukijumlisha zote za Kiswahili na Kiingereza ni Wamtumainio, Milele Daima, Adonai, Testimony na nyingine; na sasa nina Liseme na nimetoa albumu nyingine mpya ya sita ambayo ni mpya.

“Hiyo ina siku kadhaa sasa kwa hivyo za Kiswahili ni sita na za kilugha kama tatu hivi,” anasema.

Muimbaji huyo anasali katika kanisa la Anglikana ambapo mume wake ni mchungaji na anasema: “Ombi langu ni kwamba namwamini Mungu nitaendelea katika huduma yangu ya uimbaji hata kama nitakuwa na miaka 80 hata kama nitakuwa na miaka 90.

“Nitaendelea kumwimbia Mungu na kuwa mnyenyekevu na mtiifu mbele zake sio mbele za watu tu.
“Katika utunzi wangu ninamhusisha Mungu zaidi ya mimi mwenyewe ninavyojiona “Siwezi kusema ooh kwa sababu nina albumu tisa au 10; yaani nina ujuzi kabisa wa utunzi kwa hivyo simhitaji Roho Mtakatifu na simhitaji Mungu-siwezi kumsahau Mungu.
 Sarah K
“Ninawajenga watu mioyo yao; nitakuwa nawainua watu mioyo yao ambao ni wadhaifu kwenye maeneo ambayo Roho Mtakatifu ananipa watasikia wameinuka na kuwa na matarajio kwamba Mungu yupo na ataendelea kuwatendea makuu-ni mengi tu wacha niachie hapo kwanza.”

Muimbaji huyo anawataka wasanii wachanga wasife moyo na wafuatilie ndoto zao na maono yao kwa sababu kuna mambo mengi ambayo yanaweza kupotosha uimbaji wao.

“Mambo mengi huja kwa mtindo kwamba umefika kumbe bado hujafika; nitakutolea mifano miwili: hili linaweza kuzungumziwa kwa urefu sana katika uimbaji, inaweza ikaja ukiwa mchanga halafu Mungu akakupa kibali sana mbele ya watu kwa wimbo wako kupendwa na ukauzwa sana.

“Sasa hapo kikwazo kimoja kinaweza kukufanya ukarudi nyuma; ni zile hela utakazozipata kutoka kwenye uimbaji ule zinaweza kukutikisa ukarudi nyuma ukakosa kufuatilia yale maono yako uliyokuwa nayo au ahadi ulizoweka mbele za Mungu.

“Unajua kuna ahadi zile uliweka wakati uko chini kabisa ukamwambia Mungu, ‘Utakaponivusha, utakaponibariki nitafanya mambo kadhaa’; kwa hivyo unajikuta umesahau.

“La pili ni ile umaarufu wakati wimbo wako ume-‘hit’ ukajulikana sana kuna ule umaarufu unaoupata kila mtu anakuita Sarah K, Sarah K kila mtu anaongea juu yako redio zote zinakutaja; kwa hiyo hiyo umaarufu ukishaingia ndani yako na ukaukubali kwamba wewe ni maarufu ndipo kiburi kitaanza kujiinua.

“Ni vema kuendelea kuwa mnyenyekevu tu daima na umshukuru Mungu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...